Uongozi wa Yanga SC umetangaza kuwa hii ni Wiki ya Mwisho kwa Mwaka wa Fedha ndani ya timu hiyo ya Mtaa wa Twiga na Jangwani, Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi
wa Masoko, Mashabiki na Wanachama wa timu hiyo Ibrahim Samuel amesema “
Hii ni Wiki ya Mwisho kwa Mwaka wa Fedha kwetu sote wana Yanga SC.
“June
30,2025 ndiyo itakuwa tamati ya makusanyo yote ya ADA kwa wanachama
kabla ya kuukaribisha mwaka wetu wa Fedha ifikapo July 1,2025” alisema
Ibrahim.
Ibrahim aliongeza kuwa “Kama mwanachama utakuwa bado
haujalipa ADa yako mpaka June 30 basi utalazimika kulipa na msimu
unaofuata ifikapo July 1,2025 kama Ibara ya 13:3 ya katiba ya klabu yetu
inavyoelekeza.
Alifafanua kuwa “ Kama tawi lako litashindwa
kufikisha wanachama НАI 100+ hadi June 30,2025, basi litakosa uwakilishi
wa viongozi watano katika mkutano Mkuu wa msimu 2024 - 2025 kama Ibara
ya 62 ya katiba yetu inavyoelekeza.
“ Na hii ndio tofauti ya Yanga SC na vilabu vingine vyote vya Afrika Mashariki, kati na Kusini” alisema Ibrahim.
Mkurugenzi huyo ametoa kauli Mbiu ya ulipaji Ada ya Mwanachama na kusema ADA ndio nguzo Mama ya Maendeleo kwa klabu yao.
Tags
Michezo