MSANII R KELLY AGOMEWA KUACHIWA GEREZANI

 MKONGWE wa muziki wa R&B, Robert Kelly maarufu kama R.Kelly, amekataliwa ombi lake la kuachiwa kutoka gerezani siku chache baada ya mawakili wake kudai kuwa alizidishiwa dawa kutokana na njama ya kumuua iliyokwama.

 Timu ya mawakili wa nyota huyo wa zamani wa R&B iliwasilisha ombi Juni 17, ikitaka apewe kifungo cha nyumbani badala ya kusalia gerezani kutokana na 'tishio la moja kwa moja la maisha yake.'

Hata hivyo, Jaji Martha Pacold ameamua kuwa 'hakuna msingi wa kisheria kwa mahakama kushughulikia ombi hilo' na kulitupilia mbali.

Mawakili wa Kelly walidai wiki iliyopita kuwa msanii huyo alizidishwa dawa baada ya walinzi wa gereza kumpa makusudi dozi kubwa ya dawa kupuga wasiwasi na maumivu.

Pia walidai R. Kelly mwenye umri wa miaka 58, ambaye jina lake halisi ni Robert Sylvester Kelly aliondolewa hospitali kwa nguvu licha ya madaktari kugundua kuwa kulikuwa na tatizo kwenye damu yake na miguuni ambako anatakiwa kufanyiwa upasuaji.

Waendesha mashtaka wa serikali walikataa madai hayo wakati huo wakisema ni 'mambo yasiyo na maana' na wakasema ombi la hivi karibuni linadhihaki mateso waliyopitia waathirika matukio ya unyanyasaji wa ngono ambayo nyota huyo aliyafanya enzi zake.

Hata hivyo, mawakili wake walidai, 'kila muuaji, mbakaji na gaidi aliyepatikana na hatia atakuwa na nafasi mpya ya kupata uhuru' kama Kelly angeachiwa. Pamoja na hilo na kukataliwa kwa ombi la kifungo cha nyumbani, wakili wake Beau Brindley alisisitiza kwamba yeye na timu yake ya sheria wangewasilisha ombi jipya wakidai kuwa kuna 'ushahidi mpya uliogunduliwa.'

Brindley alisema ombi hilo pia litaomba dhamana ya haraka wakati shauri hilo likiendelea na kwamba, " Hatukushangazwa na uamuzi huu kwa kuwa tulijua kuwa suala la mamlaka ya kiufundi lingekuwa changamoto katika mazingira haya."

Brindley akizungumza na USA TODAY, alisema: "Awali, hata hivyo, hatukuwa na chaguo bali kuchukua hatua mara moja kutokana na ushahidi wa wazi wa tishio kwa maisha ya Robert Kelly."

Post a Comment

Previous Post Next Post

Contact Form