MMOJA ANYONGWA IRAN KUJIHUSISHA NA ISRAEL

Wakati mapigano kati ya Israel na Iran yakiingia siku ya kumi na moja, Mahakama ya Nchini humo imemhukumu kunyongwa mtu mmoja aliyepatikana na hatia ya kufanya ujasusi wa Israel. 

Kwa mujibu wa Taarifa ya Idara ya Mahakama ya Iran imeleza kuwa mtu huyo aliyefahamika kwa jina la Mohammad- Amin amenyongwa siku ya leo Jumatatu.

"Mohammad-Amin Mahdavi Shayesteh alinyongwa asubuhi ya leo kwa ushirikiano wa kijasusi na utawala wa Kizayuni," ilisema Idara ya Mahakama.

Shayesteh alidaiwa kuwa na uhusiano na Mossad, shirika la kijasusi la kigeni la Israel.

Pia alikutwa na hatia ya kushirikiana na Iran International, kituo cha televisheni cha lugha ya Kiajemi kilichoko London ambacho kinaikosoa serikali ya Iran.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Contact Form