Wakati 
mapigano kati ya Israel na Iran yakiingia siku ya kumi na moja, Mahakama
 ya Nchini humo imemhukumu kunyongwa mtu mmoja aliyepatikana na hatia ya
 kufanya ujasusi wa Israel. 
Kwa mujibu wa Taarifa ya Idara ya 
Mahakama ya Iran imeleza kuwa mtu huyo aliyefahamika kwa jina la 
Mohammad- Amin amenyongwa siku ya leo Jumatatu.  "Mohammad-Amin 
Mahdavi Shayesteh alinyongwa asubuhi ya leo kwa ushirikiano wa kijasusi 
na utawala wa Kizayuni," ilisema Idara ya Mahakama. 
Shayesteh alidaiwa kuwa na uhusiano na Mossad, shirika la kijasusi la kigeni la Israel.
Pia
 alikutwa na hatia ya kushirikiana na Iran International, kituo cha 
televisheni cha lugha ya Kiajemi kilichoko London ambacho kinaikosoa 
serikali ya Iran.