Katibu Mkuu 
wa Umoja wa Vijana wa CCM, Ndugu Jokate Urban Mwegelo (MNEC) amesema 
Amesema, Daraja hili halihusiani tu na usafiri au Usafirishaji, bali 
daraja hili ni Fursa. Kwetu sisi Vijana tunaiona miradi hii kama fursa 
ya Ajira za muda mfupi na muda mrefu, kuongeza masoko ya kibiashara, 
fursa za kidigitali na Ubunifu.
 Ndugu Jokate ameyasema hayo jana 
juni 22, 2025 katika Kongamano la Jukwaa la Fikra lililoandaliwa na 
Mwananchi Communications Limited (MCL) kwa kushirikiana na Wizara ya 
Ujenzi, lililojadili mada isemayo, 'Kujenga Madaraja, Kujenga Taifa, 
Miundombinu kama Kichocheo cha Ukuaji JumuishiNdugu Jokate 
agusia namna Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2025/30 ilivyojielekeza 
kugusuia mambo ya Kimkakati na kuigusa jamii katika ngazi ya msingi. 
“Mimi nadhani ni wakati sasa wa kuwa na mpango wa Taifa wa kuwezesha 
Vijana kushiriki katika miradi ya ujenzi wa miundombinu ya Tanzania”. 
Pamoja
 na hayo, Ndugu Jokate ampongeza Rais Samia kuwa; “Rais Samia ni 
kielelezo na tafsiri halisi ya neno Kiongozi kwa sababu hakua mbinafsi 
ameweka maslahi ya Taifa mbele, na hili kwetu sisi Vijana lazima 
tujifunze; ametufundisha kwamba unaweza kuwa Kiongozi Mwanamke, Msikivu,
 Madhubuti lakini pia mwenye uthubutu wa kufanya maamuzi magumu.”