JOKATE AFUNGUKA KUWA MSINGI WA MAENDELEO UNATOKANA NA VIJANA

 Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM, Ndugu Jokate Urban Mwegelo (MNEC) amesema Amesema, Daraja hili halihusiani tu na usafiri au Usafirishaji, bali daraja hili ni Fursa. Kwetu sisi Vijana tunaiona miradi hii kama fursa ya Ajira za muda mfupi na muda mrefu, kuongeza masoko ya kibiashara, fursa za kidigitali na Ubunifu.

 Ndugu Jokate ameyasema hayo jana juni 22, 2025 katika Kongamano la Jukwaa la Fikra lililoandaliwa na Mwananchi Communications Limited (MCL) kwa kushirikiana na Wizara ya Ujenzi, lililojadili mada isemayo, 'Kujenga Madaraja, Kujenga Taifa, Miundombinu kama Kichocheo cha Ukuaji Jumuishi

Ndugu Jokate agusia namna Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2025/30 ilivyojielekeza kugusuia mambo ya Kimkakati na kuigusa jamii katika ngazi ya msingi. “Mimi nadhani ni wakati sasa wa kuwa na mpango wa Taifa wa kuwezesha Vijana kushiriki katika miradi ya ujenzi wa miundombinu ya Tanzania”.

Pamoja na hayo, Ndugu Jokate ampongeza Rais Samia kuwa; “Rais Samia ni kielelezo na tafsiri halisi ya neno Kiongozi kwa sababu hakua mbinafsi ameweka maslahi ya Taifa mbele, na hili kwetu sisi Vijana lazima tujifunze; ametufundisha kwamba unaweza kuwa Kiongozi Mwanamke, Msikivu, Madhubuti lakini pia mwenye uthubutu wa kufanya maamuzi magumu.”




 

Post a Comment

Previous Post Next Post

Contact Form