MAAFISA UGANI 1701 WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU KUKABILIANA NA MABADILIKO YA TABIANCHI

SERIKALI kupitia Wizara ya Kilimo imeendesha mafunzo kwa Maafisa ugani 1701 kuhusu kukabiliana na mabadiliko ya Tabianchi na jinsi ya kutumia tehama katika kutoa huduma za ugani kupitia mfumo wa M-Kilimo.

 
Mafunzo hayo ni ya awamu ya kwanza yalianza tarehe 14 Aprili 2025 na kuhitimishwa tarehe 20 Juni 2025, na yamesimamiwa na Bi. Paschalina Hayuma ambaye ni mratibu wa mafunzo kutoka Wizara ya Kilimo, ambapo amesema kuwa malengo ya mafunzo haya ni kuwafikia Maafisa ugani 4,000 ifikapo 2026/2027.

Aidha amesema kuwa Mfumo wa M-Kilimo utawawezesha Maafisa Kilimo kuwasiliana na wakulima wengi kwa muda mfupi, huku wakulima wakipata taarifa mbalimbali zinazohusiana na mazao na kuwa mfumo huo utasaidia kupata taarifa ya hali ya hewa, ili kulima kilimo kinacho stahimili mabadiliko ya tabianchi.

Hii ni awamu ya kwanza ya mafunzo ambayo yamepangwa kutolewa kwa awamu tatu awamu ya pili itakuwa mwaka wa fedha wa 2025/2026 na awamu ya tatu itakuwa ni mwaka wa fedha 2026/2027, kupitia utekelezaji wa Program ya Uhimilivu wa Mifumo ya Chakula Tanzania (TFSRP) unaotekelezwa na Wizara ya Kilimo.

Maafisa ugani waliokuwa mafunzoni katika vituo vya mafunzo vya MATI Uyole, MATI Igurusi na MATI Inyala wameshukuru kupata mafunzo hayo na kuahidi kuyafanyia kazi na kuhakikisha Malengo ya Program ya TFSRP ya kufikia wakulima 3,000,000 yanafikiwa kama ilivyopangwa kufikia Agenda 10/30.







 

Post a Comment

Previous Post Next Post

Contact Form