Vijana zaidi
ya elfu sita miatano wanatarajia kupatiwa ajira kwenye sekta ya
uchimbaji wa madini ya dhahabu Nyazaga Geita chini ya uongozi wa Rais
Samia,Perseus Mining imewekeza takribani dola milioni 523 katika Mradi
wa Dhahabu wa Nyanzaga-Geita (NGP), unaotarajiwa kutoa dhahabu ya kwanza
katika Robo ya Kwanza ya 2027 kwa mtindo wa mgodi wa wazi (open-pit).
Uwekezaji huo unafadhiliwa kupitia mikopo isiyo na riba kutoka kwenye
fedha na dhahabu ya Perseus yenye thamani ya dola milioni 801. Kazi za
awali zimetekelezwa ikiwemo ujenzi wa kambi za muda, kazi za ardhi, na
utekelezaji wa Mpango wa Uhamishaji Makazi (RAP). Awamu ya kwanza ya
mgodi itadumu kwa miaka 11, ikiwa na akiba ya dhahabu inayokadiriwa
(Probable Ore Reserve) ya tani milioni 52 kwa kiwango cha 1.40 g/t, sawa
na zaidi ya 2.3 milioni oz za dhahabu. Uzalishaji unatarajiwa kuwa kati
ya 200,000 hadi 246,000 oz kila mwaka, na gharama ya uzalishaji kwa oz
(AISC) ni dola 1,211 Ikiwa thamani ya dhahabu itakuwa dola 2,100 kwa oz.
Hata hivyo Mradi wa NGP unatarajiwa kuleta faida ya fedha taslimu (free
cashflow) ya dola milioni 1,133 kabla ya kodi na dola milioni 706 baada
ya kodi. Thamani ya sasa ya mradi (NPV) inakadiriwa kuwa dola milioni
404 kabla ya kodi na dola milioni 202 baada ya kodi, huku kiwango cha
faida cha mradi (IRR) kikiwa asilimia 26 kabla ya kodi na asilimia 19
baada ya kodi, Mradi wa Nyanzaga-Geita utazalisha ajira jumla ya 6,500
za moja kwa moja.