MANARA AKUTANA NA MUFTI MKUU AMUOMBEA DUA KUELEKEA UCHAGUZI MKUU

 Wakati kampeni za Uchaguzi Mkuu zikiendelea kupamba moto katika maeneo mbalimbali ya nchi, CEO wa Manara TV na Mgombea Udiwani wa Kata ya Kariakoo, Haji Manara jana alipata nafasi ya kumtembelea Sheikh Mkuu na Mufti wa Tanzania, Sheikh Dkt. Abubakar Zuber Bin Ally, nyumbani kwake Magomeni jijini Dar es Salaam.

‎Katika ziara hiyo, Manara alimuomba Mufti dua na baraka ili safari yake ya kisiasa iwe ya amani na yenye mafanikio.

‎Mazungumzo yao pia yaligusia umuhimu wa mshikamano wa kitaifa na kudumisha maadili ya kidini wakati wa mchakato wa uchaguzi.

‎Haji Manara alisisitiza kuwa viongozi wa dini wana nafasi kubwa katika kuhakikisha siasa zinabaki kuwa chombo cha mshikamano badala ya mgawanyiko.

‎Ziara hiyo imeonekana kama hatua ya kuimarisha heshima kwa viongozi wa dini na kuonyesha mshikamo wa kijamii katika kipindi hiki cha kampeni.





 

Post a Comment

Previous Post Next Post

Contact Form