UCHIMBAJI WA KISIMA WAANZA UTEKELEZAJI WA AHADI YA SAMIA KILOSA-MOROGORO

Na Ally Mandai. 

 Siku ya tarehe 30 Agosti 2025, wakati wa kampeni za mgombea wa CCM, Ndugu Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika eneo la Mtumbatu, Wilaya ya Kilosa, Mkoa wa Morogoro, wananchi waliomba maji safi na salama.Mgombea Dkt. Samia aliwaahidi kuwachimbia kisima cha maji ndani ya siku mbili.

Leo, 31 Agosti 2025, utekelezaji wa ahadi hiyo umeanza rasmi. Wataalamu wa Wizara ya Maji wamefika eneo la Mtumbatu asubuhi na wameanza kupima miamba. Mashine ya uchimbaji itafika saa nane mchana ili kuanza kazi ya kuchimba kisima kirefu kwa ajili ya kuhudumia wananchi wa eneo hilo.

Pichani: Wataalamu wa Mkoa na Wizara ya Maji wakitekeleza agizo la mgombea wa CCM Ndugu Dkt. Samia Suluhu Hassan.



Post a Comment

Previous Post Next Post

Contact Form