VIWANJA VISIVYOFANYIWA USAFI KIGAMBONI KUTAIFISHWA

 Halmshauri ya Manispaa ya Kigamboni imeyaagiza Makampuni, Taasisi na Wananchi wote ambao wanamiliki viwanja vya matumizi mbalimbali ndani ya Manispaa ya kigamboni kuwa wanatakiwa kufanya usafi kwenye viwanja vyao ndani.

ya siku 7 kuanzia leo August 07,2025 na baada ya siku 7 kupita Manispaa itafanya ukaguzi na itachukua hatua za kisheria ikiwemo kutoza faini na kutaifisha viwanja vyote vilivyotelekezwa, huu ukiwa ni utekelezaji wa agizo la Mkuu wa Wilaya hiyo Dalmia Mikaya (@dalmiamikaya) alilolitoa July 24 , 2025 alipokagua shughuli za usafi katika maeneo mbalimbali ya Kigamboni.

Taarifa iliyotolewa leo August 07,2025 na Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini wa Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni, Joseph Semkiwa, imesema “Baada ya muda huo wa siku 7 kupita Manispaa itafanya ukaguzi na itachukua hatua za kisheria kwa wale wote ambao hawajavifanyia usafi viwanja vyao ikiwa ni pamoja na kutoza faini, kufuta umiliki au kuvitaifisha viwanja vyote vilivyotelekezwa kwa mujibu
wa sheria ya Ardhi namba 4 ya mwaka 1999 kifungu cha (44-55), Kigamboni safi ni Mimi na Wewe”

Itakumbukwa DC Dalmia Mikaya alitoa maagizo kwa Halmashauri hiyo kuhakikisha inafanya ufuatiliaji kwa Wamiliki wa viwanja na mashamba ili wafanye usafi ili kupunguza uwingi wa mapori makubwa yanayosababisha Wahalifu kuyatumia kufanyia uhalifu na pia kuleta mazingira hatarishi kwa Wananchi.

Akiongea Julai 24, 2025 wakati wa ziara yake ya ukaguzi katika maeneo ya feri Kigamboni, DC Dalmia alisema ni wajibu wa kila Mwananchi kutunza mazingira ili kujikinga na magonjwa ya mlipuko yanayoweza kuzuilika kwa kufanya usafi wa mara kwa mara huku akiwaonya pia wanaochafua maeneo ya stendi na wanaogeuza maeneo ya fukwe kuwa madampo akisema hilo halikubaliki na pia aliagiza daladala zote ziwe na vindoo vya takataka (dustbin).

Post a Comment

Previous Post Next Post

Contact Form