Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi
Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema kuwa Taifa la Tanzania mpaka kufikia
2024 ndilo deni dogo la taifa dogo kwa ukanda wa Afrika Mashariki
ukilinganisha na wastani wa deni hilo kwa nchi zote za Afrika Mashariki.
Dkt.
Samia Ameyasema hayo hii leo Agost 28, wakati akizungumza katika
ufunguzi wa kampeni za Chama cha Mapinduzi (CCM) kitaifa zilizozinduliwa
katika viwanja vya Tanganyika Pakers, Jijini Dar es Salaam ambapo
amesema kuwa deni zima la mataifa yote duniani limefika asilimia 93.
“Ndugu
wananchi deni la taifa hadi kufikia mwaka 2024, Deni la serikali zote
duniani lilikuwa asilimia 93 ya pato lote la dunia ukichukua serikali
zote za dunia, wakati pato la serikali zote za Afrika lilikuwa silimia
67 ya pato lote ndani ya bara la Afrika, kwa ukanda wa Afrika Mashariki
deni hili lilifika asilimia 67 kwa wastani wa pato la taifa kwa nchi
zote za Afrika Mashariki”
“Wakati tukienda kwa nchi Moja moja
hapa kwetu nchini Tanzania lilisalia kuwa asilimia 46 ya pato letu la
taifa na hili ndio deni dogo kuliko yote kwa nchi za Afrika Mashariki,
Asilimia 46 ukilinganisha na washtani wa asilimia 67” Amesema Dkt. Samia
Suluhu Hassan.