SALUM MWALIM KUGOMBEA URAIS KUPITIA CHAUMMA

 Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) kimemtangaza rasmi Salum Mwalim Juma kuwa Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwezi Oktoba mwaka huu.

 Tangazo hilo limetolewa leo katika Mkutano Mkuu wa Taifa wa Chama hicho unaoendelea katika Ukumbi wa Mlimani City, Jijini Dar es Salaam.

Mkutano huo umewakutanisha viongozi wa kitaifa, wajumbe wa chama kutoka mikoa mbalimbali pamoja na wanachama na wafuasi wa CHAUMMA waliokusanyika kwa ajili ya kujadili na kuamua juu ya mwelekeo wa chama kuelekea uchaguzi mkuu wa 2025.

Katika hotuba ya kutangaza uteuzi huo, Mwenyekiti wa CHAUMMA, alisema kuwa uteuzi wa Salum Mwalim umezingatia rekodi yake ya kisiasa, uadilifu, maono ya maendeleo, na uwezo wa kuunganisha Watanzania kutoka makundi mbalimbali.

Aliongeza kuwa chama kinamwamini Salum Mwalim kuwa ndiye mgombea bora wa kuleta mageuzi ya kweli ya kiuchumi, kijamii na kisiasa kwa Tanzania.

Salum Mwalim Juma, ambaye aliwahi kuwa mwanasiasa kijana mashuhuri na naibu katibu mkuu wa chama kimoja kikuu cha upinzani kabla ya kujiunga na CHAUMMA, amekuwa mstari wa mbele katika kupigania haki za wananchi, utawala bora na uwajibikaji wa viongozi serikalini.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Contact Form