FATMA FEREJ MGOMBEA MWENZA WA URAIS TANZANIA BARA

 Chama cha ACT-Wazalendo kimekamilisha safu yake ya juu ya wagombea wa nafasi ya urais kwa upande wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kumteua Ndugu Fatma Abdulhabib Ferej kuwa Mgombea Mwenza wa urais wa Luhaga Mpina ambaye amechaguliwa kuwania Urais katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu.

Uteuzi huo umetangazwa rasmi  wakati wa Mkutano Mkuu wa chama hicho, ambapo wajumbe walipitisha jina la Ferej kwa kauli moja kufuatia mapendekezo ya Kamati Kuu ya chama.

‎Fatma Ferej ni Katibu wa Ngome ya Wanawake ya ACT-Wazalendo, na ana rekodi ndefu ya uongozi serikalini na ndani ya chama.

‎Ameshawahi kuwa Mbunge, Mwakilishi wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, pamoja na kuhudumu kama Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar.

‎Kwa uteuzi huo, Ferej atashirikiana na mgombea urais wa chama hicho, Ndugu Luhaga Mpina, kuongoza kampeni ya ACT-Wazalendo kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Contact Form