RAIS SAMIA AMVUA UBALOZI WA CUBA,HUMPHREY POLEPOLE

 Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imethibitisha kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, ametengua uteuzi wa Balozi Hamphrey Polepole, aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Cuba, na kumwondolea rasmi hadhi ya ubalozi.

Taarifa hiyo imetolewa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dk. Samwel Shelukindo, kufuatia barua rasmi iliyopokelewa kutoka kwa Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dk. Moses Kusiluka.

Kwa mujibu wa barua hiyo, Rais Samia, kwa kutumia mamlaka aliyopewa chini ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kwa mujibu wa sheria ya utumishi wa umma, amechukua hatua mbili kuu dhidi ya Polepole Kutengua uteuzi wake kama Balozi wa Tanzania nchini Cuba, Kumuachisha kazi rasmi kwa manufaa ya umma

Taarifa hiyo imeeleza kwamba, hatua hizo zimeanza kutekelezwa rasmi kuanzia tarehe 16 Julai 2025.

Hamphrey Polepole, ambaye aliwahi kushika nyadhifa mbalimbali za juu serikalini na ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), alikuwa amepelekwa kuiwakilisha Tanzania nchini Cuba kama balozi, nafasi aliyoshika hadi uteuzi wake ulipotenguliwa.

Wizara ya Mambo ya Nje imeeleza kuwa hatua nyingine za kiutumishi na kidiplomasia kuhusu nafasi hiyo zitatolewa kwa wakati muafaka, kadri taratibu za uteuzi mpya zitakavyokamilika.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Contact Form