ACT WAZALENDO KUFANYA MKUTANO MKUU KITAIFA

 Chama cha ACT Wazalendo kinatarajia kufanya Mkutano Mkuu Maalum wa Taifa siku ya Jumatano, tarehe 06 Agosti, 2025, katika Ukumbi wa Mlimani City, jijini Dar es Salaam.

 Mkutano huu utafanyika kwa mujibu wa Ibara ya 61 ya Katiba ya ACT Wazalendo ya Mwaka 2015, Toleo la mwaka 2024, ambayo inatoa mamlaka ya kuitisha Mkutano Mkuu kwa ajili ya maamuzi muhimu ya chama.

Kabla ya Mkutano Mkuu, kutafanyika vikao vya Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya Taifa, ambavyo vitafanyika siku ya Jumanne, tarehe 05 Agosti, 2025, katika Ukumbi wa Hakainde Hichilema uliopo Makao Makuu ya Chama.

Mkutano huo Maalum umeitishwa kwa lengo kuu la kufanya uteuzi wa wagombea wa nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na Zanzibar, kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Contact Form