IFCU YAISAIDIA AMCOS KUANZISHA HUDUMA ZA KIFEDHA

Chama Kikuu cha Ushirika Mkoa wa Iringa (IFCU) kimeendelea kutoa mafunzo kwa wanachama wa vyama vya ushirika (AMCOS) yanayolenga kuanzisha huduma ndogo za kifedha na kupunguza ukatili wa kijinsia. 

Akizungumza wakati wa semina hiyo Agost 5, 2025 Ukumbi wa Maktaba, Manispaa ya Iringa, Mhasibu wa IFCU Mkoa wa Iringa Flora Mwaipungu amesema mafunzo hayo ni muhimu ili wanachama waamke kiuchumi kwa kuanzisha SACCOS ndogo au kuimarisha zile zilizopo na hivyo kuongeza kipato cha kaya zao.

Amesema pia mafunzo yanasaidia kuhakikisha wanachama wanakuwa na usawa wa kijinsia katika AMCOS zao.

Naye Afisa Maendeleo Manispaa ya Iringa Ester Sanga smesisitiza umuhimu wa wanachama kuwa na huduma ndogo za kifedha wa kujiunga kwa pamoja  ili kukuza kipato cha kaya, kuanzisha biashara, kufanya kilimo cha kisasa na kuondoa mikopo umiza yenye riba kubwa inayodai giza kwenye madeni na kuwadidimiza kiuchumi.

Aidha amewataka wanachama kupeleka elimu kwa wengine na kuhakikisha hakuna ukatili wa kijinsia ili kutoa fursa sawa kwa wote.

Kwa upande wao Wanachama walioshiriki wamekishukuru chama kikuu cha ushirika Mkoa wa Iringa (IFCU) kwa mafunzo hayo kwani  yametoa motisha kwa wanaume na wanawake kushirikiana katika kuanzisha huduma ndogo za kifedha na kutoa taarifa za ukatili katika maeneo yao huku akisisitiza umuhimu wa kushirikiana kikamilifu katika kuboresha kipato na huduma za kifedha za wanachama.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Contact Form