HIZI HAPA SABABU KUU TATU ZA LUHAGA MPINA KUHAMIA ACT WAZALENDO

 Mwanasiasa mkongwe na aliyewahi kuwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Joelson Mpina, amejiunga rasmi na chama cha upinzani cha ACT Wazalendo, hatua inayotajwa kuibua mvutano wa kisiasa kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2025.

 Mpina, ambaye alihudumu kama Mbunge wa Jimbo la Kisesa kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa miaka kadhaa, ameonekana katika picha na video zilizosambaa mitandaoni, akijiandikisha kupitia mfumo rasmi wa chama hicho uitwao Kiganjani, mbele ya Naibu Kiongozi wa ACT Wazalendo – Taifa, Dorothy Semu. Taarifa hizo sasa zimethibitishwa na uongozi wa chama hicho.

Kwa hatua hiyo, Mpina anakuwa mmoja wa viongozi waandamizi wa zamani wa CCM waliokihama chama hicho na kujiunga na ACT Wazalendo katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi, hatua ambayo wachambuzi wa siasa wanaiona kama "kuongeza uzito wa kisiasa kwa ACT Wazalendo."

Mpina amekuwa akitajwa na watu wa karibu kuwa hakuridhishwa na mwelekeo wa ndani ya CCM, hasa kuhusu misingi ya uwajibikaji na usimamizi wa rasilimali za umma, mambo aliyokuwa akiyasimamia kwa sauti kubwa alipokuwa bungeni na serikalini.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Contact Form