WAGOMBEA 208 WAJITOKEZA KUCHUKUA FOMU MOROGORO MJINI,UDIWANI NA UBUNGE

 Idadi ya Watia nia 208 wamejitokeza kuchukua fomu nafasi ya udiwani kwenye kata 29 za wilaya ya Morogoro Mjini ambapo nafasi ya ubunge ni wagombea 17 pekee. Akizungumza katika ofisi za CCM Wilaya ya Morogoro mara baada ya kukamilika kwa mchakato wa uchukuaji na urejeshaji wa fomu Katibu wa Chama Cha Mapinduzi wilaya ya Morogoro Mjini Twalibu Kassimu Berege ametoa mchanganuo wa idadi ya wagombea nafasi ya udiwani katika kata zote.


Kati ya wagombea ubunge 17 katika jimbo la Morogoro mjini 3 ni wanawake na 14 ni wanaume huku nafasi ya wagombea udiwani kati ya 208 wanawake 39 na wanaume 169”. “Wananchama wameweza kujitokeza kwa wingi kuchukua fomu katika nafasi ya udiwani  na mchanganuo wao ni kama ifuatavyo :kata ya Tungi 9,Mindu 14 Chamwino 10,Mwembesongo 5 ,Kilakala 7,Mafisa 10,Kauzeni 6,Sabasaba 3 Kiwanja cha ndege 6,Kihonda 8,Bigwa 5,Uwanja wa Taifa 11,Magadu 6,Kichangani 7,Mafiga 7,Kingo 3,Mazimbu 4,Mkundi 8,Sultani 3,Kihonda maghorofani 15 Lukobe 10,Boma 6,Mlimani 8,Kingolwira 9,Lubungo 11,Mji mkuu 4,Mji mpya 4 na Mzinga 6.”            

Ameongeza kuwa “kutamatika kwa zoezi hilo kunatoa nafasi ya kuanza kwa vikao vya mchujo kwaajili ya kuwajadili wagombea na kutoa mapendekezo ambapo tarehe 4 wataanza ngazi ya kata na tarehe 6 ngazi ya wilaya na kuendelea kwahiyo tunawataka wanachama waliochukua fomu na kugombea waendelee kuwa watulivu waamini vikao ngazi ya kata,wilaya na ngazi ya mkoa kwa uteuzi nafasi ya madiwani na Taifa kwa ngazi ya Ubunge tunategemea kwamba chama kitawaletea watu wazuri watu watakokwenda kufanya ushindani kwenye soko la siasa la chama cha mapinduzi na wapinzani kwahiyo tunategemea watu tutakaowarudisha watauzika”. 

Kwa upande wa Jumuiya za chama cha mapinduzi wamejitokeza wanachama kuchukua na kurejesha fomu ambapo Jumuiya ya Umoja Wa Vijana wa CCM mkoa wamejitokeza wanachama 5 kuchukua fomu na 4 kati yao wamefanikiwa kurejesha huku 1 akishindwa kurejesha fomu,Jumuiya ya Umoja wa wanawake Tanzania wamejitokeza wanachama 31 kuchukua na wote wamerejesha pamoja na Jumuiya ya Wazazi wamejitokeza wanachama 2 kuchukua na kufanikiwa kurejesha.





Post a Comment

Previous Post Next Post

Contact Form