RAIS WA MPITO WA MALI AJIPA MUDA USIO NA KIKOMO MADARAKANI

 

Rais wa Mpito wa Mali, Assimi Goita, ametia saini sheria mpya inayompa mamlaka ya kubaki madarakani kwa muda usio na kikomo. Sheria hiyo imeondoa ukomo wa mihula ya urais na kuchelewesha uchaguzi mkuu, hatua ambayo imeibua hofu kubwa miongoni mwa wakosoaji kuhusu mustakabali wa demokrasia nchini humo.

Wapinzani na wanaharakati wa haki za kiraia wanasema hatua hiyo ni kurudi nyuma kwa maendeleo ya kidemokrasia, huku wakihofu kuwa Mali inaweza kutumbukia katika utawala wa kiimla. Hadi sasa, haijabainika lini uchaguzi mpya utafanyika.

Goita, alichukua madaraka kupitia mapinduzi ya kijeshi mwaka 2021, sasa anashikilia mamlaka makubwa zaidi, huku jumuiya ya kimataifa ikitoa wito wa kurudishwa kwa utawala wa kiraia.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Contact Form