MAHAKAMA YATUPILIA MBALI MAOMBI YA LISSU

 Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Dar es Salaam, imetupilia mbali maombi ya Mwenyekiti wa Chadema, Tundu Lissu, aliyekuwa akitaka uamuzi wa Mahakama ya Kisutu wa kuahirisha usikilizwaji wa kesi yake ya kuchapisha taarifa za uongo mtandaoni upitiwe upya.

 

Katika uamuzi wake, Mahakama Kuu imesema kuwa maombi hayo hayakuwa sahihi kufikishwa kabla ya kesi ya msingi kukamilika, hivyo yamekataliwa kwa msingi wa kisheria.

Tundu Lissu alikuwa anapinga uamuzi uliotolewa Juni 2, 2025, na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, lakini sasa atalazimika kusubiri hadi kesi ya msingi itakapokamilika ndipo hatua zaidi ziweze kuchukuliwa.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Contact Form