MWANZA WAPIGWA MSASA UTUNZAJI WA MAZINGIRA

 Katika juhudi za kuimarisha usafi wa mazingira na kuleta mabadiliko chanya katika Jamii, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa kushirikiana na Halmashauri zake wamehitimisha ziara ya kimafunzo Mkoani Iringa ikiwa lengo ni kujifunza kwa nadharia na Vitendo juu ya mifumo ya usimamizi wa usafi wa mazingira, ushirikishwaji wa jamii, na mbinu za kuzuia magonjwa ya mlipuko. 

Ziara hiyo ambayo ilikuwa ni ya siku 4 imehitimishwa July 22, 2025 katika Halmshauri ya Wilaya ya Iringa, Kijiji cha Ufyambe Timu hiyo kutoka Mwanza ambayo imejumuisha Afisa Afya wa Mkoa, Katibu wa Afya wa Mkoa, pamoja na Waganga Wakuu wa Halmashauri za Mkoa pamoja na Maafisa Afya kutoka Halmashauri za Jiji la Mwanza, sengerema, misungwi na llemela.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Dkt. Jesca Lebba amesema ziara hiyo itakwenda kuleta tija ambapo kupitia uzoefu huo walioupata utatumika kuleta maboresho ndani ya Mkoa wa Mwanza.

"Mkoa wa Iringa umekuwa ni moja ya Mikoa ambayo inafanya vizuri katika zile tatu bora Tanzania na sisi Mwanza mazingira yetu na Iringa yanafanana tunataka na sisi kuboresha katika maeneo yetu ili kuzuia magonjwa ya mlipuko" amesema Lebba

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Iringa Silvia Mamkwe amesema kutokana na Mkoa wa Iringa kufanya Vizuri katika afua ya Mazingira imekuwa mfano wa kuigwa ambapo imehakikisha imefikia kaya zaidi ya asilimia 98 zimefanikiwa kuwa na Vyoo lakini pia kaya zaidi ya asilimia 95 kuwa na vyombo vya kunawia mikono.

Aidha amesema kuwa Mafanikio hayo yanatokana na ushirikiano mkubwa wa Wananchi pamoja na Uongozi wa Mkoa huku akitoa wito kwa Wakazi wa Iringa kuhakikisha wanaendelea kutunza mazingira ili kuendelea kuwa kinara wa usafi kitaifa.




 

Post a Comment

Previous Post Next Post

Contact Form