MAJALIWA AMALIZA ZIARA BELARUS,ANADI FURSA ZA UWEKEZAJI

 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa ametumia ziara yake nchini Belarus kunadi fursa za uwekezaji katika maeneo manne ya kipaumbele ya Serikali ya Awamu ya Sita ambayo ni Kilimo, Afya, Madini na Ulinzi na Usalama.

 Mhe. Waziri Mkuu katika siku mbili za ziara yake, tarehe 22 na 23 Julai 2025 ametembelea kampuni kubwa nane zenye nguvu ya mitaji jijini Minsk na kuzihakikishia utayari wa Serikali ya Tanzania kushirikiana nazo kwa kuzipatia kila aina ya msaada zitakapokuja Tanzania kuwekeza.


Kwenye eneo la Kilimo, Mhe. Waziri Mkuu alikutana na viongozi wa Kampuni ya AFTRADE ambayo tayari ipo nchini na kuwasisitiza kuongeza kasi katika kuendeleza Kilimo hususan kuwa na programu za kuwasaidia Wakulima wadogo mitaji, utafiti na mafunzo ili Kilimo kiweze kuwa na tija, kizalishe ajira na kuongeza usalama wa chakula nchini.

Katika eneo hilo la Kilimo, Waziri Mkuu pia alitembelea chuo cha Kilimo cha Belarus na Viwanda vya Matrekta na kuvishawishi viwanda hivyo kufungua matawi nchini Tanzania.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Contact Form