HAJI MANARA APITISHWA NA KAMATI KUU CMM

 Chama Cha Mapinduzi (CCM) kupitia Kamati ya Halmashauri Kuu ya Chama hicho, imemteua Mkurugenzi Mtendaji wa Manara TV, @hajismanara , kuwa miongoni mwa wagombea watakao wania nafasi ya Udiwani katika Kata ya Kariakoo,Wilaya ya Ilala, Jijini Dar es Salaam.

Uteuzi wa Manara umetokana na mchakato wa kina wa ndani wa chama ambapo wagombea kadhaa walichujwa kwa mujibu wa taratibu na vigezo vilivyowekwa na CCM.

Manara ameibuka miongoni mwa waliokidhi vigezo na kuaminiwa na chama hicho ambapo wengine wagombea walioteuliwa kuwania nafasi hiyo ni pamoja na Daudi Abdallah Simba,Abdulkarimu Massamaki.

Uamuzi huu wa CCM pia unaonekana kuwa majibu kwa tetesi na mijadala iliyokuwa imeenea mitandaoni na kwenye baadhi ya vyombo vya habari kuhusu jina la Manara kutokupitishwa na Kamati Kuu ya chama.

Uteuzi huu sasa unaweka wazi msimamo wa chama na kuondoa sintofahamu kwa wanachama na wafuasi wa CCM.

Haji Manara si jina geni ndani ya chama hicho, akiwa amewahi kushika nafasi mbalimbali za uongozi, ikiwemo kuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, nafasi iliyompatia umaarufu mkubwa kutokana na ustadi wake wa kuwasiliana na wanachama pamoja na wananchi.

Mbali na siasa, Manara anafahamika pia kwa mchango wake mkubwa katika tasnia ya michezo nchini, hususan alipokua Msemaji mahiri wa vilabu Vikubwa nchini Simba SC na Yanga SC.




Post a Comment

Previous Post Next Post

Contact Form