KESI YA TUNDU LISSU YAHAIRISHWA MPAKA AGOSTI 13

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imepanga Agosti 13, 2025 kutoa uamuzi juu ya hoja zilizoibuliwa baina ya Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu na Upande wa Serikali katika kesi ya uhaini.

Kesi ya Lissu ilitajwa leo mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi, Franko Kiswaga ambapo Jopo la Mawakili wa Upande Jamhuri uliongozwa na Nassoro Katuga, huku Lissu akijitetea mwenyewe.

Mbali na hoja nyingine, Lissu aliiomba mahakama hiyo kutupilia mbali kesi hiyo ikiwezekana kuifuta kutokana na Upande wa Jamhuri kuichelewesha licha ya upelelezi kukamilika.

“Kwa mara ya kwanza naomba uwaambie mahakama hii isiahirishe kesi, huu mchezo ni ukatili sana, nipo mahabusu ninaishi na wafungwa waliohukumiwa kifo ili nianze kuzoea zoea, wakatilie mheshimiwa ama kesi ifutwe,”.

Kwa upande wake wakili Katuga aliiomba mahakama hiyo iahirishe kesi kwa kuwa wanasubiri uamuzi wa Agosti 4, 2025 katika Mahakama Kuu ya Tanzania juu ya hatma ya maombi yao ya kuwalinda mashahidi kama yatakubaliwa ama la.

“Mahakama Kuu imepanva kutoa uamuzi ambao tunausubiri ili tuwasilishe taarifa kwani mahakama yako haiwezi kutoa amri kwa Mahakama Kuu hivyo hatuna budi kusubiri maamuzi hayo,”.

Kutokana na mvutano huo uliochukua takribani saa moja na nusu, Hakimu Kiswaga alisema;

“Leo hii sitatoa maamuzi madogo nitaahirisha na sababu ni kwamba imekuwa kawaida natiaga maamuzi hapa hapa ila mawasilisho ya leo yamekuwa ni yale ambayo yanawasilishwaga hapa na hata kesi zilizotumika pia, hivyo mahakama inahitaji muda. Naahirisha kesi hadi tarehe 13, 8, 2025,”.

Katika kesi hiyo, Lissu anakabiliwa na shtaka moja la uhaini akidaiwa kutenda kosa hilo April 3, 2025 kwa madai ya kuhamasisha kuzuia Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.



Post a Comment

Previous Post Next Post

Contact Form