AZIZ KI HUYO ANARUDI YANGA,WYDA WAKUBALI YAISHE

 Sakata la mchezaji Stephanie Aziz Ki limechukua sura mpya huko Wydad Casablanca baada ya sintofahamu kuibuka juu ya yeye kuendelea kuchezea timu hiyo au kuna jambo lingine litaendelea.

Meneja habari na mawasiliano wa klabu ya Yanga SC, Ali Kamwe ametoa ufafanuzi juu ya mkataba wa kiungo huyo Aziz Ki na klabu ya Wydad Casablanca na kueleza kuwa makubaliano yao ilikuwa ni kuwatumikia Wydad kwa mkataba wa miezi mitatu.

Ali Kamwe ameweka wazi kwamba, mkataba huo una vipengele viwili ambapo ikiwa Wydad Casablanca itaridhishwa na kiwango chake basi watamuongezea mkataba wa miaka miwili na ikiwa tofauti na hapo atarejea ndani ya Yanga SC na kuendelea na mashindano mwingine.

Yanga SC na Wydad walikubaliana hadi kufikia Julai 10, wawe wameshawasiliana ili kuona kama kuna kuongeza mkataba au kuishia hapo.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Contact Form