CCM IRINGA YAWAFUNDA WENEZI KATA 28

Chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Iringa Vijijini kimeendesha mafunzo maalum kwa makatibu wa siasa na uenezi kutoka kata zote 28 za wilaya hiyo yakilenga kuwaandaa kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 kupitia uelewa wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2025-2030. 

Akizungumza katika mafunzo hayo Katibu wa Siasa na Uenezi wa CCM wilaya hiyo Anold Hezron Mvamba amewataka wenezi hao kusoma na kuielewa kwa kina Ilani ya Uchaguzi ya chama hicho akisisitiza kuwa imegusa maeneo muhimu kama kilimo, afya, elimu na nishati.

“Ilani hii lazima iwafikie wananchi kwa usahihi ili kufanikisha ushindi wa kishindo kwa CCM katika uchaguzi mkuu ujao,” amesema Mvamba.

Mvamba ameongeza kuwa mafanikio yaliyopatikana chini ya uongozi wa Mwenyekiti wa CCM Taifa Rais Samia Suluhu Hassan ni ushahidi tosha wa utekelezaji mzuri wa Ilani hivyo ni wajibu wa makatibu hao kuwa mabalozi wa kueleza maendeleo hayo.

Kwa upande wake Katibu wa CCM wilaya ya Iringa Vijijini Bi. Sure Mwasanguti aliwataka wenezi hao kuielewa vyema Katiba ya chama pamoja na maelekezo mbalimbali ya chama hasa kuelekea uchaguzi Mkuu.

Mgeni rasmi katika mafunzo hayo, Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Iringa Vijijini, Ndugu Constantino Kihwele aliwahimiza makatibu wenezi kutambua wajibu wao kwa chama na kuepuka kubeba wagombea kabla ya mchakato rasmi wa uteuzi.

“Chama chetu kitapata wagombea bora watakaoiwakilisha CCM kwa ufanisi katika nafasi zote,” alisema huku akiwahimiza makatibu hao kuendelea kuwaeleza wananchi mafanikio ya serikali ya awamu ya sita na kusisitiza kuwa kazi kubwa iliyofanywa na Rais Samia ni msingi wa ushindi mkubwa wa chama katika uchaguzi ujao.

“Chini ya uongozi wa Rais Samia, bendera ya CCM itapepea kwa kura za kishindo




Post a Comment

Previous Post Next Post

Contact Form