MAPENZI YA JINSIA MOJA BURKINAFASO,JELA MIAKA MITANO

 Bunge la mpito la Burkina Faso limepitisha rasmi sheria mpya inayoharamisha mapenzi ya jinsia moja, na kuanzisha adhabu ya kifungo cha hadi miaka mitano jela.

Sheria hiyo, iliyopendekezwa kwa mara ya kwanza Julai 2024, iliidhinishwa rasmi na kuanza kutumika Septemba 1, 2025 Chini ya sheria hiyo mpya, wahalifu wanakabiliwa na kifungo cha kati ya miaka miwili na mitano pamoja na faini.

Waziri wa Sheria Nchini humo Edasso Rodrigue Bayala alieleza kuwa hatua hiyo inatumika sio tu kwa raia lakini pia kwa raia wa kigeni, ambao pamoja na vifungo vya jela wanaweza kukabiliwa na kufukuzwa. 


 

Post a Comment

Previous Post Next Post

Contact Form