YANGA YAMTAMBULISHA KIUNGO CONTE KUTOKA CS SFAXIEN YA TUNISIA

 Kiungo Moussa Balla Conte leo ametambulishwa rasmi kuwa mchezaji mpya wa Klabu ya Yanga SC, akitokea CS Sfaxien ya Tunisia, baada ya kusaini mkataba wa miaka mitatu wa kuwatumikia Wananchi.

Awali, usajili wa Conte uliibua sintofahamu kubwa, huku ripoti mbalimbali za vyombo vya habari zikimhusisha na Simba SC, ambapo ilidaiwa alikuwa karibu kutua Msimbazi. Hata hivyo, Yanga SC imeibuka kidedea katika vita ya kumsajili kiungo huyo, baada ya kumtambulisha rasmi na kuthibitisha kuwa huduma ya kiungo huyo sasa ni mali ya Wananchi kuelekea msimu mpya wa mashindano.





 

Post a Comment

Previous Post Next Post

Contact Form