PSSF KUFANYA UWEKEZAJI KWENYE MAENEO YENYE TIJA

 Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), umewekeza maeneo salama yenye kuuwezesha kupata faida kubwa ikiwemo hati fungani na dhamana za Serikali na kwa mwaka wa fedha uliomalizika wamepata faida ya trilioni 1.3.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Mipango, Uwekezaji na Miradi PSSSF, Bw. Fortunatus Magambo kwenye banda la Mfuko huo kwenye Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam yanayoendelea kwenye viwanja vya Julius Nyerere, maarufu Sabasaba Julai 7, 2025.

Amesema asilimia 84 ya uwekezaji uliofanywa na mfuko huo umewekwa maeneo hayo ya hati fungani ambako kuna uhakika unaoouwezesha Mfuko kupata faida kubwa na kulipa wastaafu na wanachama wake mafao mazuri na endelevu.

“Tumewekeza maeneo salama maeneo ambayo yanaleta faida kubwa kwa wakati ili tuweze kulipa mafao bora kwa wastaafu wetu na wanachama, ndiyo maana asilimia 84 ya uwekezaji wetu tumeuwekeza kwenye amana za serikali na hati fungani,” alisema Bw. Magambo.

Ameongeza kuwa “Tunapokea wafanyakazi wapya kila siku na wengine wanastaafu kwa hiyo wakistaafu wanapaswa wakutane na pensheni yao, ili iwe hivyo lazima tuwekeze fedha zao kwenye maeneo sahihi yenye faida ya haraka na ya uhakika na uwekezaji huu unafuata miongozo ya Benki Kuu ya Tanzania BoT,” alisema

Pia amewahakikishia wanachama wa PSSSF wakiwemo wastaafu kuwa Mfuko uko salama una ukwasi wa kutosha kuhakikisha mafao yanalipwa kwa wakati siku zote.

Aidha Kagaruki alimpongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuweka mazingira mazuri ya biashara ambayo yamesababisha jengo hilo refu zaidi kupata wateja kwa asilimia 80.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Contact Form