Mkuu wa 
Wilaya ya Lindi, Victoria Mwanziva ameendelea na ziara ya kikazi ya kata
 kwa kata katika kuwafikia wananchi wa wilaya hiyo kwa ukaribu na 
kutimiza adhma mbalimbali kwa mujibu wa ratiba yake ikiwa ni pamoja na 
Kuwa na mkakati maalum wa kusikiliza na kutatua changamoto mbalimbali za
 wananchi pamoja na Muendelezo wa ukaguzi wa utendaji wa watendaji wa 
serikali na kukagua, kuweka mawe ya msingi, kutembelea na kuzindua 
miradi mbalimbali iliotekelezwa chini yake Serikali ya awamu ya sita.
Aidha,
 Mhe Victoria ameendelea na ukaguzi wa miradi ya maendeleo ambapo 
amepata nafasi ya kufanya ukaguzi wa umaliziaji wa Ujenzi wa mabweni 
mawili katika shule ya Sekondari Nangaru- yenye thamani ya 103,727,096 
na kuweka jiwe la msingi katika mradi huo sambamba na kuzungumza na 
watumishi, wanafunzi na wananchi waishio eneo jirani.
Akiendelea 
na ziara yake, Sambamba na hapo DC Mwanziva amekagua Ujenzi wa madarasa 3
 na matundu 6 ya vyoo shule ya Msingi Makumba ambapo pia ameweka jiwe la
 msingi katika mradi huu wenye gharama ya 83,200,000 na kupokelewa kwa 
kishinda na wanachi wenye hamasa kubwa baada ya kupokea mradi huo.
Katika
 hatua nyingine, Akizungumza na wananchi waliojitokeza katika maeneo ya 
Mradi DC Mwanziva amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 
Mheshimiwa Dkt Samia Suluhu Hassan kwa maendeleo makubwa ambayo 
wana-Lindi wanaendelea kupata na kunufaika katika nyanja na Sekta 
mbalimbali zikiwemo Elimu, Afya, Miundombinu na Kilimo.