DC MWANZIVA NA ZIARA YA KATA KWA KATA MKOANI LINDI

 Mkuu wa Wilaya ya Lindi, Victoria Mwanziva ameendelea na ziara ya kikazi ya kata kwa kata katika kuwafikia wananchi wa wilaya hiyo kwa ukaribu na kutimiza adhma mbalimbali kwa mujibu wa ratiba yake ikiwa ni pamoja na Kuwa na mkakati maalum wa kusikiliza na kutatua changamoto mbalimbali za wananchi pamoja na Muendelezo wa ukaguzi wa utendaji wa watendaji wa serikali na kukagua, kuweka mawe ya msingi, kutembelea na kuzindua miradi mbalimbali iliotekelezwa chini yake Serikali ya awamu ya sita.

Aidha, Mhe Victoria ameendelea na ukaguzi wa miradi ya maendeleo ambapo amepata nafasi ya kufanya ukaguzi wa umaliziaji wa Ujenzi wa mabweni mawili katika shule ya Sekondari Nangaru- yenye thamani ya 103,727,096 na kuweka jiwe la msingi katika mradi huo sambamba na kuzungumza na watumishi, wanafunzi na wananchi waishio eneo jirani.

Akiendelea na ziara yake, Sambamba na hapo DC Mwanziva amekagua Ujenzi wa madarasa 3 na matundu 6 ya vyoo shule ya Msingi Makumba ambapo pia ameweka jiwe la msingi katika mradi huu wenye gharama ya 83,200,000 na kupokelewa kwa kishinda na wanachi wenye hamasa kubwa baada ya kupokea mradi huo.

Katika hatua nyingine, Akizungumza na wananchi waliojitokeza katika maeneo ya Mradi DC Mwanziva amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt Samia Suluhu Hassan kwa maendeleo makubwa ambayo wana-Lindi wanaendelea kupata na kunufaika katika nyanja na Sekta mbalimbali zikiwemo Elimu, Afya, Miundombinu na Kilimo.




 

Post a Comment

Previous Post Next Post

Contact Form