CHALAMILA AMALIZA MGOGORO WA WAFANYABIASHARA

 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Albert Chalamila leo Julai 12,2025 amemaliza mgogoro wa jumuiya ya wafanyabiashara wa Manzese na Halmashauri ya Ubungo ambao umetokana na wafanyabiasha hao kushindwa kulipa Ushuru wa Huduma "Service Levy" ambao ulipelekea wafanyabiasha hao kufunga maduka 11 wakidai Serikali iwatoze ushuru huo kwa "flat rate"

RC Chalamila amesema Serikali chini ya uongozi mahiri wa Dkt Samia Suluhu Hassan inawathamini wafanyabiasha na siku zote Rais ameendelea kuweka mazingira rafiki ya kufanya biashara, hivyo kwa kuwa Ushuru wa Huduma uko kisheria ni vigumu kubadili takwa hilo la kisheria kwa sasa ni lazima wizara husika ihusishwe hivyo ni mchakato.

Kwa mantiki hiyo RC Chalamila amewataka wafanyabiasha hao kuandika maelezo ya kuomba kupewa muda maalum wa kukamilisha deni hilo ili timu ya watalaam wa biashara ikae ione namna bora ya wafanyabiasha hao tena mmoja mmoja atakavyoweza kulipa deni hilo bila kuathiri biashara yake.

Aidha RC Chalamila amekemea tabia ya uanaharakati kwenye biashara, "migomo haina tija kamwe usidanganyike kuwa katika vikundi kugoma, biashara ni ya mtu mmoja mmoja na sio kikundi " Alisema RC Chalamila.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Contact Form