AZAM FC YAMREJESHA TENA AISHI MANULA

 Klabu ya Azam FC imetangaza rasmi kukamilisha usajili wa nyanda Aishi Manula kutoka Simba SC alikodumu kwa miaka minane. Usajili huu umekamilika kwa uhamisho huru, na Manula amesaini mkataba wa miaka miwili hadi mwaka 2027.

Manula mwenye miaka 29 aliondoka Azam FC mwaka 2017 na kujiunga na Simba SC, ambako alifanikiwa kutwaa mataji mbalimbali ya ndani na kufika robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika mara kadhaa. Hata hivyo, nafasi yake kikosini ilianza kuyumba baada ya kuumia nyonga mwishoni mwa msimu wa 2022/23, hali iliyomuweka nje kwa miezi sita. Katika msimu wa 2023/24, alicheza mechi chache tu, huku makipa wengine kama Ayoub Lakred na Moussa Camara wakipewa nafasi zaidi .

Azam FC, waliomaliza nafasi ya pili katika Ligi Kuu ya Tanzania msimu uliopita na kufuzu kwa Ligi ya Mabingwa Afrika, wanahitaji uzoefu na uongozi wa Manula katika safu ya ulinzi. Ujio wake unatarajiwa kuimarisha kikosi hicho, hasa katika mashindano ya kimataifa na ya ndani .

Kwa sasa, Manula anatarajiwa kuwa kipa chaguo la kwanza wa Azam FC kwa msimu wa 2025/2026, akichukua nafasi ya Mohamed Mustafa ambaye alisumbuliwa na majeraha msimu uliopita.

Kwa mashabiki wa Azam FC, kurejea kwa Manula ni habari njema na ishara ya dhamira ya klabu hiyo kutwaa mataji na kufanya vizuri katika mashindano ya kimataifa.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Contact Form