ZIJUE DONDOO MUHIMU KUHUSU KIWANDA CHA KWANZA CHA KUCHENJUA SHABA CHA MAST- CHUNYA MBEYA



KUANZISHWA
Mineral Access Systems Tanzania Ltd (MAST) ni Kampuni ya Kitanzania, iliyoanzishwa mwaka 2011, ikiwa na dhamira ya kuendeleza biashara ya madini kwa njia shirikishi na endelevu. Imekuwa ikifanya biashara ya madini ya kimkakati (strategic minerals) ndani na nje ya nchi mfano Zambia, Congo, Zimbabwe na South Africa, hususan shaba, nikeli na manganese, kwa kushirikiana na wachimbaji wadogo katika mikoa mbalimbali nchini.

UWEKEZAJI
Kiwanda cha MAST - Chunya ni matokeo ya uwekezaji wa zaidi ya dola milioni 10 za Kimarekani (USD) ikiwa ni uwekezaji wa ubia kati ya Kampuni ya MAST na MCC kutoka New York, Marekani.

LENGO LA KUANZISHWA
Kuchenjua madini ya shaba yenye kiwango cha chini 0.5 hadi asilimia 2 yanayopatikana katika eneo hilo la Mbugani Chunya na kuyapandisha thamani kufikia hadi asilimia 75 (copper cement) kwa kutumia teknolojia ya leaching na cementation.

UWEZO WA SASA WA UZALISHAJI
Kwasasa kiwanda kina uwezo wa kuchakata takriban tani 31,200 za mashapo ya shaba kwa mwezi, ambapo tani 27,200 zitatoka katika mgodi wa kampuni hiyo ya MAST, na tani 4,000 zitanunuliwa kutoka kwa wachimbaji wadogo nchini.

MPANGO WA UJENZI WA VIWANDA VINGINE NCHINI
MAST ina mpango wa kujenga viwanda vingine vitatu vya uchenjuaji katika mikoa ya Manyara-Simanjiro, Ruvuma-Mbesa (Tunduru), na Dodoma, kila kimoja kikitarajiwa kutoa ajira zaidi ya 500 na kuchochea athari za kiuchumi zenye thamani ya USD milioni 40 kwa mwaka.

MPANGO WA UANZISHAJI MITAMBO MINGINE
Kiwanda kimejipanga kuanzisha mitambo maalum ya usindikaji wa nikeli kwa ajili ya kushughulikia aina zote mbili mbale za madini ya Nikeli ambazo ni laterite na sulfide. Hatua hii inalenga kutekeleza kwa vitendo dhamira ya kitaifa ya kuongeza thamani ya madini yote yanayochimbwa ndani ya mipaka ya nchi.

AJIRA ZILIZOZALISHWA HIVI SASA
Tayari kiwanda kimetoa ajira kwa wafanyakazi 254, wakiwemo 209 waajiriwa moja kwa moja wa MAST na 45 kupitia wakandarasi. Kati ya hao, watanzania 205 wamenufaika moja kwa moja ambao takriban ya asilimia 60 ya hao wakitoka Mkoa wa Mbeya, Wilaya ya Chunya.


Post a Comment

Previous Post Next Post

Contact Form