MULIRO ASEMA KILA MTU ANAPASWA KUWA MLINZI WA MWENZAKE

 Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam Jumanne Muliro amesema washiriki wa Maonesho ya 49 Biashara ya Kimataifa (DITF) ili kuzuia uhalifu katika maonesho hayo kila mtu anapaswa kuwa mlinzi wa mwenzake.

 

Amesema kila mmoja anapaswa kuzingatia sheria, miongozo na kanuni zilizoandaliwa na waandaaji wa maonesho hayo ili kuzuia uhalifu.

Hayo ameyasema siku ya jana Juni 26, 2025
jijini Dar es Salaam Muliro wakati akitoa mada katika semina ya kuwajengea uwezo washiriki wa maonesho hayo iliyoandaliwa na Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade).

"Kila mtu anapaswa kuwa mlinzi wa mwenzake na kwamba ili ulinzi uweze kufanyika vizuri ni lazima watu watii sheria, kanuni na taratibu zilizopo katika maonesho haya," amesema.

Kamanda Muliro amesema ni muhimu washiriki wa maonesho hayo kuepuka kubeba mizigo isiyojulikana au yenye mashaka pamoja na kuchukua tahadhari vya vitu vyenye asili ya mlipuko.

“Washiriki wote ni muhimu mkazingatia sheria na kanuni za maonesho, pia mtoe taarifa haraka kwa walinzi endapo kuna hali ya hatari pamoja na kufuata miongozo yote ya ulinzi iliyoandaliwa na waandaaji,” amesema

Pia amesisitiza kuwa hakuna maendeleo yanyaoweza kutokea bila kuwepo kwa mazingira salama na kwamba ulinzi hutoa msingi wa uwekezaji wa kibiashara, elimu bora na huduma za afya na miundombinu salama.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Contact Form