KITENDO cha
Simba kushinda 5-0, kimemfanya kipa namba moja wa kikosi hicho, Moussa
Camara kujihakikishia tuzo ya Kipa Bora wa Msimu kwa kufikisha clean
sheet 18, ambazo zinaweza kufikiwa na Djugui Diarra pekee, ambaye
anaweza kufanya washindi wa tuzo hiyo kuwa wawili msimu huu.Hata
hivyo, hiyo ni kama tu Diarra ambaye ana clean sheet 16, hataruhusu bao
katika mechi mbili zilizobaki na Camara akashindwa kutoruhusu bao
katika mechi mbili zijazo.
Hata
hivyo, hiyo ni kama tu Diarra ambaye ana clean sheet 16, hataruhusu bao
katika mechi mbili zilizobaki na Camara akashindwa kutoruhusu bao
katika mechi mbili zijazo.
Hii inamaanisha Camara
ameshajihakiishia kumaliza kinara, na endapo Diarra akimfikia, Tanzania
itakuwa na makipa bora wawili kama England msimu huu.
Pia golikipa huyu wa klabu ya Simba anawania tuzo ya Golikipa Bora wa mwaka wa Guinea katika tuzo za CIS Media Moussa Camara anawania tuzo hiyo na Mory Keita (Hafia Fc), Mohamed Camara (Asante Kotoko), Sekou Sylla (Horoya), na Yero Diallo (Renaissance).
Tags
Michezo