MADIWANI 11 WA CCM WANG'OLEWA MOROGORO

 Watia nia 11 waliongoza kwenye kura za maoni za Udiwani kupotia Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Morogoro wameondolewa.

 Wakati zoezi la mchujo katika chama Cha Mapinduzi likiendelea nchini Tanzania kwa Mkoa Morogoro watia nia 11 waliongoza katika kura za maoni udiwani kupitia chama hicho wameondolewa kwa kushindwa kukidhi baadhi ya vigezo

Akitoa taarifa yake kwa waandishi wa habari ,katibu mkuu wa chama Cha Mapinduzi (CCM ) Mkoa wa Morogoro ndugu Nuru John Ngereja amesema kuwa sababu za kutoteuliwa kwa wagombea hao ni pamoja uvunjifu wa maadili,makundi ndani kwenye kata zao.

Aidha ndugu Ngereja amezitaja Kata sita ambazo ni Mindu,Mwembesongo,Lukobe,Kilakala,Mbuyuni na Mlimani kuwa bado zinasubiri maamuzi kutoka kamati maalumu ya Chama Cha Mapinduzi CCM Manispaa ya mkoa wa Morogoro.

Katibu wa CCM ndugu Ngereja amesema kuwa wagombea wote walioongoza nafasi ya udiwani viti maalumu wameteuliwa kwenye nafasi hizo.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Contact Form