HAJI MANARA AUTAKA UDIWANI KARIAKOO

Mkurugenzi Mtendaji wa Manara Tv,Haji Sunday Manara ambaye pia ni Kada Maarufu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Manara Leo Julai 01, 2025 amechukua rasmi fomu ya kuwania Udiwani katika kata ya Kariakoo iliyopo Jimbo la ilala Jijini Da es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa Habari mara baada ya kukabidhiwa fomu hiyo na Katibu jumuiya ya wazazi CCM Kata ya Kariakoo Bi. Shum Gessan, @hajismanara amesema kuwa yeye ni mzaliwa wa Kariakoo na amechukua fomu hiyo kuomba ridhaa ya kuongoza Wananchi wa Kariakoo na viunga vyake.

Haji Manara ni miongoni mwa makada wakongwe wa Chama cha Mapinduzi na amewahi kutumikia chama hicho katika ngazi mbalimbali ikiwemo kuwa Katibu Mwenezi katika Mkoa wa Dar es Salaam.




 

Post a Comment

Previous Post Next Post

Contact Form