ENOCK BELLA AMUOMBA MBOSSO MSAMAHA HADHARANI

 Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Enock Bella, ameomba radhi hadharani kwa mwimbaji Mbosso kufuatia mahojiano aliyoyafanya mwaka jana ambapo alimuelezea vibaya. Enock Bella amesema kuwa alikosea kama kijana na anatambua kosa lake, hivyo anaomba msamaha kwa Mbosso na kwa Watanzania wote walioumizwa na maneno yake.

 

"FIRST, kaka yangu na ndugu yangu Mbosso kwanza nichukue nafasi hii kuomba RADHI hadharani kwa kukukwaza kwenye mahojiano niliyofanya mwaka jana, kama binadamu siwezi kuwa sawa siku zote na ndio ubinadamu kwa hilo nabeba uwajibikaji na naomba RADHI.

Kama ulivyosema ROOM NUMBER MOJA ( YAMOTO BAND) ilikuwa si tu band bali shule nzima ya maisha na viongozi wetu walitufundisha kusaidiana, kuchukuliana madhaifu, kuwajibika na kuomba radhi ukiteleza, hivyo ndugu yangu NIWIE RADHI,

Watanzania wapenzi wa Mbosso na Enock Bella nawaomba pia radhi kwa kukwazika sisi bado ni vijana wenu wenye ndoto za kupambania na supporters wetu ni nyie hivyo kwa lilitokea mniwie radhi kijana wenu na muendelee kutupa support na tuendelee kuenjoy miziki mizuri iliyo ndani ya ROOM NUMBER THREE.

Ndugu zangu wa media naomba sana, sitakuwa na mahojiano tena kuhusu suala hili kwangu nimelimaliza hapo , ndugu yangu amesema nilichomkwaza na ninaomba radhi hivyo sina maoni mengine juu ya interview ya kaka yangu Mbosso.

 tutafutane kwa maswali mengine ila si kwa swala hili "🙏 

Mbosso naye akaja akajibu Hivi,

 "Kipindi Wenzetu Wawili Wametangulia Kupata Management na Kuachia Kazi Zao na Wakiwa Wanafanya Shows zao .. Mimi na Wewe Ndo Tulikuwa Tunaongea Muda Mwingi ndani pale Maskani Tabata Savanna…
Niliacha Mziki na Sikuwa Nataka Mziki Kabisa Baada ya Kuona Ya Moto Band imevunjika .. ila Siku niliokukuta Unalia Chumbani Peke Yako na Ukasema ‘ Nakunukuu “.. Mbosso Fanya Mziki Wewe Utanisiadia Naujua Moyo Wako ..” Nilikusikiliza na niliamua Kuanza Tena Mishe mishe Za Miziki na kwa Baraka Za Mungu Neema zilianza na nilichagua kushare na wewe Kwenye Kidogo na Kikubwa nilichopata ..,
Nilifanya Hivyo Kaka Kuanzia Kwenye Shows zangu Hadi Kwenye Maisha Ya Kawaida Kwa Ujumla … Unajua Kwa Nini …? Kwa Sababu Kauli Yako Moja ilitosha Sana Kunipa ujasiri na Leo Nipo Hapa …

Love You so Much Bro ❤️🫂

Post a Comment

Previous Post Next Post

Contact Form