STEVE BARKER ATAJA MALENGO MATATU SIMBA,MAPINDUZI CUP 2026

Na Ally Mandai 

Kocha Mkuu wa Simba, Steve Barker, amesema anaianza michuano ya Kombe la Mapinduzi 2026 akiwa na malengo makuu matatu.

Barker amesema kwanza anaitumia kuwafahamu vizuri wachezaji, pili ni sehemu ya kujiandaa na mashindano mengine yanayokuja ikiwamo Ligi ya Mabingwa na tatu kubeba taji la Mapinduzi.


Simba iliyopo Kundi B, kesho Januari 3, 2026 itaanza kwa kucheza dhidi ya Muembe Makumbi City kwenye Uwanja wa New Amaan Complex, Unguja, kisha Januari 5, 2026 itaikabili Fufuni, ikiwa mechi ya mwisho hatua ya makundi.

Baada ya michuano hiyo, Simba ina mechi za Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Esperance ya Tunisia, ikianzia ugenini Januari 23, 2026, kisha nyumbani Januari 30, 2026.

Katika Ligi ya Mabingwa, mechi mbili za kwanza Simba imepoteza, hivyo inaburuza mkia wa kundi D.



 

Post a Comment

0 Comments