Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameagiza
vyombo vya Ulinzi na Usalama pamoja na Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka
(DPP) kuchuja kwa makini mashtaka ya vijana walioshtakiwa kwa kosa la
uhaini kufuatia maandamano ya Oktoba 29, 2025.
Akihutubia Bunge
leo tarehe 14 Novemba 2025, Rais Samia alisema kuna kundi kubwa la
vijana waliokamatwa bila kuelewa uzito wa kile walichokifanya, huku
wengine wakijihusisha katika maandamano kwa kufuata mkumbo bila dhamira
ya kufanya uhalifu.
“Natambua kuna vijana wengi wamekamatwa kwa
kushtakiwa kwa makosa ya uhaini—hawakujua wanachokifanya na wengine
wamefuata mkumbo. Nikiwa kama Mama, navielekeza vyombo vya kisheria
kuangalia makosa yaliyofanywa na vijana wetu. Kwa wale ambao walifanya
mambo kwa kufuata mkumbo na hawakudhamiria kufanya uhalifu, wawafutie
makosa yao.”
Akiendelea, alieleza kuwa rekodi na video za tukio
la maandamano zinaonyesha wazi kuwa baadhi ya vijana walishiriki kwa
ushabiki bila kuwa na nia ya kuvuruga amani. Kwa msingi huo, alitoa
maagizo mahsusi kwa Ofisi ya DPP:
“Naelekeza Ofisi ya DPP kuchuja viwango vya makosa, na kwa waliofuata mkumbo wawaachie waende kwa wazazi wao.”
Tags
Habari
