LISSU AIBUA MJADALA MAHAKAMANI,MAJAJI WAAMURU KIZIMBA CHA SHAHIDI WA SIRI KIREKEBISHWE

Na Ally Mandai. 

Mahakama Kuu Masijala ndogo ya Dar es imesema itafanyia marekebisho upya kizimba kilichopo ndani ya Mahakama ili Shahidi wa Siri aweze kutoa ushahidi.

Hatua hiyo imekuja baada ya pingamizi aliloliweka mshitakiwa Tundu Lissu Novemba 12,2025 baada ya kukataa shashidi wa Nne wa siri wa upande wa Serikali ambaye alikuwa anatoa ushahidi wake bila kuonekana na mtu yeyote wakiwemo majaji wenyewe.

Akitoa uamzi huo,jaji anayesimamia kesi hiyo Dustin Ndunguru amesema amri ya 3 inasema kizimba maalum ya Shahidi ni sehemu ya kukaa au kusimama akiwa anaonekana kwa majaji na kutokana na kizimba hicho kilivyo basi ni kweli Shahidi hataonekana lakini Mahakama itafanyia marekebisho kizimba hicho ili shahidi wa Siri aweze kuonekana kwa majaji kwa kuzingatia kifungu cha 194 cha ulinzi wa mashahidi.

Amesema hoja ya Mshitakiwa ya kwamba hatuweza kumhoji vilivyo Shahidi maswali dodoso (Cross Examination) kwa kutokana na uwezo wa kutomuona, Jaji Ndunguru amesema hoja hizo siyo za msingi kwani mshitakiwa atakuwa na uwezo wa kufanya hivyo.

Ikumbukwe kuwa pingamizi hilo lilitolewa Novemba 12, 2025 na mshitakiwa Tundu Lissu kumpinga shahid wa Nne wa siri wa Serikali aliyefahamika kwa jina la P11.

Kwa mantiki hiyo, Mahakama imetupilia mbali mapingamizi yote yaliyotolewa na Mshitakiwa Tundu Lissu na badala yake upande wa Mahakama itafanyia marekebisho kizimba hicho ili shahidi aweze kuonekana.

Baada ya maamzi hayo,upande wa Jamhuri uliomba kuahirishwa kwa shauri hilo,jambo ambalo lilipingwa na mshitakiwa huku akiomba mashahidi wengine waje ili kesi iendelee.

Baada ya maombi ya pande zote mbili,jopo la majaji limejadiliana na kukubaliana kuwa Shauri litaendelea kesho Alhamisi saa tatu asubuhi.




 

Post a Comment

0 Comments