RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI WA WENYEVITI WA BODI MBALIMBALI NCHINI

Na Ally Mandai. 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amefanya uteuzi wa wenyeviti wa bodi mbalimbali. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Moses Kusiluka, walioteuliwa ni kama ifuatavyo:-

(i) Mhe. Anne Samamba Makinda ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Usimamizi ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Wengine ni

(ii) Bw. Jaffer Machano ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Reli Tanzania (TRC). Bw. Jaffer anachukua nafasi ya Bw. Ally Amani Karavina;

(ii) Dkt. Albina Andrew Chuwa ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Kituo cha Taifa cha Ufuatiliaji wa Kaboni (NCMC); na

(iv) Prof. Makenya Abraham Maboko ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU).

 

Post a Comment

0 Comments