RAIS TRUMP ATHIBITISHA MAREKANI KUMKAMATA RAIS MADURO WA VENEZUELA

 Na Ally Mandai

 Marekani ilishambulia Venezuela usiku kucha na kumkamata Rais wake aliyehudumu kwa muda mrefu, Nicolas Maduro, Rais Donald Trump alisema mapema leo Jumamosi baada ya miezi kadhaa ya kumshinikiza kufuatia tuhuma za biashara ya dawa za kulevya na kukosa uhalali wa kushika madaraka.

Washington haijafanya uingiliaji wa moja kwa moja kama huo katika Amerika ya Kusini tangu uvamizi wa Panama mwaka 1989 uliolenga kumuondoa madarakani kiongozi wa kijeshi Manuel Noriega, kwa tuhuma zinazofanana.
“Marekani imefanikiwa kutekeleza shambulio kubwa dhidi ya Venezuela na kiongozi wake, Rais Nicolas Maduro, ambaye yeye pamoja na mke wake wamekamatwa na kusafirishwa nje ya nchi,” Trump alisema katika chapisho lake kwenye Truth Social.
Marekani ilikuwa imemtuhumu Maduro kuendesha “dola la mihadarati (narco-state)” na kupanga matokeo ya uchaguzi wa mwaka jana, ambao upinzani ulisema uliushinda kwa kishindo. 

Kiongozi huyo wa Venezuela, aliyerithi madaraka kutoka kwa Hugo Chavez mwaka 2013, amesema Washington inataka kudhibiti hifadhi ya mafuta ya Venezuela, ambayo ni kubwa zaidi duniani.

Post a Comment

0 Comments