MBETO :SIKU,SAA NA DAKIKA ZAMSUBIRI RAIS DK MWINYI KURUDI IKULU

Na Mwandishi Wetu, Zanzibar 

Chama Cha Mapinduzi kimesema hakitishiki  wala kustushwa na mbwembwe za upinzani  kwa kuwa kina uhakika wa  kupata ushindi mnono  kupitia masanduku ya kura  ifikapo oktoba 29  Mwaka  huu.

Katibu  wa Kamati Maalum vya NEC Zanzibar , Idara ya Itikadi ,Uenezi na Mafunzo , Khamis Mbeto  Khamis  ameeleza hayo huku akithibitisha mgombea Urais wa CCM   Rais Dk Huseein  Ali Mwinyi  atarudi ikulu kwa kishindo  .

Mbeto  alisema kuna  mambo matano muhimu yaliofanyika  katika miaka mitano ya uongozi  wa Rais  Dk Mwinyi  yatakayomfanya arudi tena ikulu kwa ridhaa ya Wananchi. 

Akiyataja masuala hayo, alisema ni kuitikiwa kwake  na wananachi wa makundi  yote ,utawala wake kupinga vitendo vya  ubaguzi , msisimko wa  maendeleo  ya aina yake  ,huku akitimiza ahadi  za chama na zake binafsi .

"Zanzibar ya sasa  sio ile ilioachwa na wakoloni  .Rais Dk  Mwinyi  ameendeleza kazi ilioanzishwa na watangulizi wake. Amezishughulikia changamoto  za msingi na  kuzipatia majibu ya kudumu  "Alisema Mbeto 

Aidha, Katibu  huyo Mwenezi  alisema kutokana na uchapakazi wake  miaka mitano iliopita,kura za ushindi wa Rais   huyo hazina shaka hivyo nguvu ya umma  itamrudisha tena madarakani  .

"Hivi sasa Zanzibar   hazitajwi changamoto  katika  sekta ya  elimu, uhaba wa madawati na  madarasa.Sasa kuna  masoko bora ,barabara za lami  ,  zahanati na hospitali zenye tiba na  dawa "Alieleza 

Mbeto akizungumzia uwajibikaji,utendaji na uwazi katika  Serikali, alisema yamefanyika mageuzi makubwa ya kimfumo pamoja na umakini katika ukusanyaji wa  mapato  ya serikali .

Pia kazi nyingine ambayo itaongeza mtaji wa kura za  Rais ni ukarabati mkubwa katika viwanja vya ndege , ujenzi wa Bandari, na kuanza  mchakato wa Uchimbaji wa Mafuta na gesi .

"Uongozi   wa Rais Dk Mwinyi umewaunganisha wananchi na kuwa jamii moja .Hakuna  malalamiko ya upendeleo maeneo ya  kazi. Kila mtumishi  huwajibika kwa  nafasi  yake" Alisema Katibu huyo Mwenezi.


 

Post a Comment

Previous Post Next Post

Contact Form