MBETO AFUNGUKA KUWA DKT.MWINYI YUKO TAYARI KUITUMIKIA TENA ZANZIBAR

Na Mwandishi  Wetu, Zanzibar 

Chama Cha Mapinduzi  kimesema Mgombea wake wa Urais Zanzibar Rais Dk Hussein Ali Mwinyi  yuko imara huku akijiandaa kutwaa ushindi  wa kidemokrasia ili kuiongoza tena Serikali ya Mapinduzi  Zanzibar  kipindi cha pili.


Vile vile,Chama  hicho kimemtaja Makamu Mwenyekiti  wa ACT  Wazalenzo, Ismail Jussa  Ladhu, atabaki kuwa legelege na tepetepe kwakuwa  hayo ndio maisha alioyachagua kuishi .

Katibu  wa kamati Maalum ya NEC  Zanzibar 5
Idara ya Itikadi,Uenezi na Mafunzo,  Khamis  Mbeto  Khamis, ameeleza hayo akijibu madai ya Jussa aliyedai kuwa Rais Dk Mwinyi yuko tepetepe kwa akihofia  kushindwa Uchaguzi  .

Mbeto  alisema kwa haiba na  ustawi wa mabadiliko ya  Maendeleo makubwa yaliochomoza  chini ya  uongozi wa Rais  Dk Mwinyi ni ujinga na upuuzi mtu kusema  kiongozi  huyo atashindwa Uchaguzi .

Alisema  siku zote Wananchi wanahitaji kuona Serikali yao ikiwatumikia kwa kuwaletea  maendeleo ikiwemo kuimarika kwa huduma za kijamii na wananchi wakifaidika nazo .

"Jussa ataendelea kuwa legelege na tepetepe kwakuwa ndio maisha ulioyachagua toka akiwa kijana mdogo. Amekubali mwenyewe kuchagua mkondo huo wa maisha  hivyo ajikubali kubaki kama ilivyo " Alisema Mbeto 

Akiuzumgumzia  uimara wa Mgombea Urais  wa CCM, Mbeto  alisema Rais Dk Mwinyi yuko imara na madhubuti huku  akisubiri siku ya kutangazwa na kuwa Rais kwa kipindi  cha pili. 

'Kwakuwa tumejiandaa kushinda lazima tuibuke na ushindi usio na longolongo.Sera za chama chetu zimejibu changamoto zote zilizokuwa zikiwatatiza wannchi katika sekta za Maendeleo  .Tumetimiza ahadi na wajibu wetu .Ni  haki  yetu kupata ushindi wa kishindo" Alisema Mbeto 

Aidha, Katibu  Mwenezi  huyo aliongeza kusema  mkataba wa miaka mitano iliopita kati ya wananchi na CCM,ni utekelezaji wa   Ilani ya Uchaguzi. Kazi hiyo kimsingi imefanyika kwa weledi  na umakini mkubwa na kukamilika" Alieleza

"Rais ametekeleza ahadi za kisera na zile zakibinafsi  hivyo hawezi  kushindwa na mgombea anayetaka achaguliwe ili akafanye majaribio ya kuongoza nchi  .Serikali si  chumba cha maabara cha kufanyia majaribio " Alisisitiza Mbeto 

Katibu huyo Mwenezi, amewahakikishia Wananchi, Wanachama wa CCM  , wafuasi na Wakeleketwa wake ,kujiandaa na kwenda kupig kura Oktoba  29 kisha wawe tayari  kupokea matokeo ya  ushindi.  

"Jussa na wenzako  jiandaeni kushuhudia kimbunga  cha ushindi  wa CCM kikiwapeperusha . Hila na njama zenu zimekwama hivyo jipangeni kutoka machozi bila kilio "Alisema katibu Mwenezi  huyo


Post a Comment

Previous Post Next Post

Contact Form