Waziri
Mkuu Kassim Majaliwa ametoa wito kwa wananchi kushiriki uchaguzi mkuu
kwa amani huku akiwahakikishia kuwa serikali itatekeleza wajibu wake
ipasavyo.
"Nitoe rai kwa kila mmoja wetu kuhakikisha kila mmoja
analinda na kuitunza tunu ya amani na utulivu wa nchi kabla wakati na
baada ya uchaguzi.”Akizungumza Bungeni leo juni 26 Majaliwa
amesema serikali imejiandaa vyema na itahakikisha inasimamia uchaguzi
ili kuwawezesha wale weye sifa waweze kuchaguliwa na hata kushiriki
kuchagua wale wanaowataka.
"serikali itahakikisha inatekeleza
wajibu wake wa kuhakikisha inatekeleza wajibu wake wa kusimamia katiba
ili kila mwananchi mwenye sifa ya kuchagua au kuchaguliwa aweze
kutekeleza haki yake ya kikatiba nila vikwazo vya aina yoyote”
0 Comments