MUSEVENI ATANGAZA NIA YA KUGOMBEA URAIS 2026

Chama tawala nchini Uganda, National Resistance Movement (NRM), kimethibitisha kuwa Rais Yoweri Museveni atagombea muhula mwingine katika Uchaguzi Mkuu wa 2026 nchini humo.

Tangazo hilo linaweka mazingira kwa Museveni kurefusha utawala wake wa takriban miongo minne nchini Uganda, nchi ambayo inamfahamu mkuu mmoja tu wa serikali tangu Januari 1986.

Kwa sasa, Museveni ni kiongozi wa nne barani Afrika aliyetawala kwa muda mrefu zaidi, huku chama tawala kikiwa kimefanyia marekebisho katiba ya Uganda mara mbili huko nyuma ili kumruhusu kuongeza muda wa utawala wake.

Mpinzani wa karibu wa Museveni atakuwa mwanasiasa Robert Kyagulanyi, maarufu Bobi Wine, ambaye alishika nafasi ya pili katika kura za mwisho za mwaka 2021 na tayari amethibitisha nia yake ya kugombea 2026.

Wakati huo huo, kiongozi mwingine mkuu wa upinzani na mpinzani wa muda mrefu wa Museveni, Dkt. Kizza Besigye, bado yuko kizuizini baada ya kutekwa nyara mjini Nairobi tarehe 16 Novemba 2024 na kusafirishwa kurudi Uganda kupitia barabara.

Besigye anakabiliwa na mashtaka mengi yakiwemo ya kumiliki silaha na uhaini.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Contact Form