Jeshi la
Polisi Mkoa wa Kilimanjaro linawashikilia watu wawili ambao ni Sharif
Abdallah Mabishi (20) na Boniface Machila (22), raia wa nchi jirani, kwa
tuhuma za wizi wa mita 14 za maji zinazomilikiwa na Mamlaka ya Majisafi
na Usafi wa Mazingira Moshi (MUWSA).
JE,HUPATI WATEJA? TANGAZA NASI KWA ELFU 5 UFIKE MAELFU PIGA SASA 0654414804.
Tukio hilo limetokea usiku
wa kuamkia leo, Agosti 22, 2026, katika Kitongoji cha Miembeni, Kata ya
Makuyuni, Mamlaka ya Mji Mdogo wa Himo, Mkoani Kilimanjaro ambapo Askari
Polisi kwa ushirikiano wa Wananchi na viongozi wa Serikali za Mtaa
walibaini uwepo wa wanaume watatu katika eneo hilo majira ya saa 8
usiku, wakiwa na mita hizo kwenye pikipiki aina ya TVS yenye namba za
usajili KMGW 960.
Katika hatua hiyo, watu wawili walikamatwa, huku
mmoja alifanikiwa kukimbia na kutokomea kusikojulikana na msako
unaendelea ili kufanikisha kukamatwa kwake.
Uchunguzi wa tukio hilo unaendelea na baada ya kukamilika, hatua nyingine za kisheria zitachukuliwa kwa mujibu wa sheria.
Jeshi
la Polisi Mkoa wa Kilimanjaro linatoa wito kwa Wananchi kuendelea
kushirikiana na Jeshi la Polisi kwa kutoa taarifa zitakazosaidia
kuwakata wahusika wa wizi wa mali za Serikali na uhalifu mwingine ili
hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao.
0 Comments