Mkuu wa
Wilaya ya Chake Chake, Zuhura Mgeni Othman, amefanya ukaguzi katika
nyumba iliyopo Chanjamjawiri, Pemba, inayodaiwa kutumika kwa shughuli za
biashara ya ngono.
Katika ukaguzi huo, zimeonekana kondomu
zinazodaiwa kuhusishwa na shughuli hizo, huku Mkuu huyo wa Wilaya
alisema kuna viashiria vinavyoashiria uwepo wa biashara ya kuuza mwili
katika nyumba hiyo.
Zuhura amesema hali hiyo inatia wasiwasi
kutokana na madai kuwa eneo hilo hutembelewa pia na vijana na watoto,
akisisitiza kuwa Serikali haitavumilia vitendo vinavyokiuka maadili ya
jamii.
Amewataka wananchi kutoa taarifa kwa vyombo vya dola
wanapobaini maeneo yanayodaiwa kutumika kwa shughuli hatarishi, huku
akisema hatua za kisheria zitachukuliwa baada ya uchunguzi kukamilika.
0 Comments