Mahakama ya
Wilaya ya Chunya imewahukumu watu wawili kifungo cha miaka 30 jela kila
mmoja baada ya kutiwa hatiani kwa makosa ya ubakaji na ulawiti
yaliyotokea maeneo tofauti wilayani humo.
GUSA HAPA,REJESHA HESHIMA CHUMBANI NA KAMA UNAHITAJI AJIRA SASA
Amos Masanja (28),
mkazi wa Igangwe, amehukumiwa miaka 30 jela kwa kumlawiti kijana wa
kiume mwenye umri wa miaka 20, tukio lililotokea Julai 7, 2026 katika
Kijiji cha Igangwe.
Hukumu hiyo imetolewa Agosti 13, 2026 na
Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Chunya, Bruno Bungole, baada ya
mahakama kujiridhisha na ushahidi uliowasilishwa.
Katika tukio
lingine, Lusekelo Kajingili (43), mkazi wa Chalangwa na baba wa kambo wa
mwathirika, amehukumiwa miaka 30 jela baada ya kutiwa hatiani kwa
kumbaka mtoto wa miaka 15, mwanafunzi wa shule ya msingi.
0 Comments