KESI YA LISSU YAAHIRIUSHWA BAADA YA SHAHIDI KUUGUA

Kesi inayomkabili Mwenyekiti wa Chama Cha upinzani CHADEMA Tundu Lissu, imeahirishwa hadi Jumatatu ya Agosti 17 baada ya Shahidi wa 18 kati ya 30 aliyetakiwa kutoa ushahidi wake leo kupata dharura ya kiafya. 

GUSA HAPA,REJESHA HESHIMA CHUMBANI NA KAMA UNAHITAJI AJIRA SASA 

Akitangaza Mbele ya jopo la majaji watatu, wakili mwandamizi wa Serikali amesema shahidi huyo amehudhuria Clinic katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili kutokana na changamoto ya kiafya.


Wamesema hata mashahidi ni binadamu, hivyo changamoto ya kiafya inaweza kumtokea yeyote huku wakiahidi kuja na mashahidi wote waliobaki Jumatatu ya Agosti 17,2026.

Hata hivyo mshitakiwa Tundu Lissu, amepinga vikali ombi hilo la upande wa Jamhuri huku akisema kuwa, wanafanya hivyo kwa vile Mahakama haichukui hatua yoyote kwani ilishatoa maelezo kwa upande wa Jamhuri kuja na mashahidi kuanzia wawili.

Mshitakiwa Tundu Lissu, amesema kama upande wa Jamhuri hauwezi kuendelea 'akitumia neno "Pumzi kukata", basi wafunge mashahidi na kuendelea hatua nyingine.

Hata hivyo jopo la majaji watatu likiongozwa na Dustan Ndunguru imekubaliana na ombi la upande wa Jamhuri na kuagiza upande wa Jamhuri kuja na mashahidi wote Jumatatu ya Agosti 17.

Lissu ambaye leo anatimiza siku 493 akiwa gerezani, jana alimhoji shahidi wa 17 wa siri aliyepewa jina la P, ambaye alianza kutoa Ushahidi wake kabla ya kufanyiwa maswali dodoso.

Lissu anakabiliwa na shtaka moja la uhaini kinyume na kifungu cha 39(2)(d) cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu, linalotokana na maneno aliyoyatamka kuhusiana na kusudio la kuzuia kufanyika kwa uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.

Post a Comment

0 Comments